Halloween party ideas 2015
Image

Na Yusuph Mwamba
KLABU  ya soka ya West Ham United imekamilisha dili la kumsajili winga wa  kimataifa wa Uturuki ,Gokhan Tore, kwa ajili ya kuitumikia klabu hiyo katika msimu ujao wa ligi kuu Uingereza maarufu kama EPL Premier League.
Tore mwenye umri wa miaka 24, aliyezaliwa Nchini Ujerumani, amefanikiwa kudumu kwa misimu miwili Uingereza huku akiitumikia timu ya soka ya Vija ya Klabu ya Chelsea kabla hajatimkia kunako klabu ya Hamburg mwaka 2011.
Usajili wa mwanandinga huyo umefanikiwa kuigharimu klabu ya soka ya West Ham United kiasi cha pauni milioni 2.5 ikiwa ni ada kwa ajili ya mkopo kutoka klabu ya soka ya Besiktas  lakini pia kutampa uhuru mwanandinga huyo kama atakubali kusaini moja kwa moja kunako klabu hiyo mwisho wa msimu baada ya mkopo kumalizika
Licha ya kupambana sana, lakini Tore hakuweza kufanikiwa kipindi akiitumikia klabu yake ya Rubin Kazan ya Nchini Russia kabla ya kujiunga na  Besiktas.
Hatua ya kumtoa mwanandinga huyo kwa mkopo ilianzia msimu wa  mwaka   2013-14 hatimaye na kupata kuwa mchezaji wa kudumu mnamo msimu wa mwaka  2014.
Hata hivyo, alifanikiwa kumaliza msimu wa ligi 2015/2016 akifanikiwa kutikisa nyavu mara 19 katika michezo  111 aliyocheza akiwa na timu yake ya  Besiktas lakini hakufanikiwa kuorodheshwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Uturuki kilichokuwepo kwenye fainali ya michuano ya kombe la Euro 2016 Nchini Ufaransa. 
" Nafurahi sana kutua West Ham, nilikuwa nikifuatilia baadhi ya michezo yao na ndio kitu ambacho kilinivutia kujiunga na klabu hii". Alisema Tore 
"Utumwa umenifanya nijiunge na klabu hii, na ndio sababu kubwa iliyopelekea kuwa hapa West Ham, kocha wao ni mtu mwenye msaada sana na mimi na mjua vizuri naye ananijua tarajieni kazi nzuri kutoka kwangu kikubwa ushirikiano ni kocha mzuri sana ni kama baba yangu na hapa ni kama familia yangu " Aliongeza Tore


JIUNGE NASI , BONYEZA HAPA http://www.wabunifumedia.blogspot.com ku-install App ya wabunifumedia,  bila ya kuingia website

Tweet@wabunifumediaonline, youtube@wabunifumediaonline TV, Fb@wabunifumediaonline, insta@wabunifumediaonline



Post a Comment

Theme images by Maliketh. Powered by Blogger.