Halloween party ideas 2015
Image

Na Issa Ramadhani
UTAFITI uliofanywa na  wanasayansi ,umeonesha  kuwa kati ya watu wa nne wenye dalili za maambukizi ya ugonjwa wa kisonono na pangusa waliotumia dawa  ya antbiotics wakipima kwa mara ya pili watatu kati ya hao hawana tena  magonjwa hayo kutokana na ubora wa dawa hizo,ila mmoja ana vimelea vya magonjwa hayo ya zinaa.
Utafiti huo ulifanywa na watafiti kutoka Hospital ya St.Johnhuko Michgani na ulijumuisha sampuli ya watu 1,103, ambao waliugua magonjwa hayo na kutumia dawa za  Antbiotics.
Watu hao ambao walitibiwa kwa dawa za antibiotics,waliporudiwa hospital na kupimwa tena baada ya magonjwa hayo.
Miongoni mwa dalili za magonjwa hayo  ya zinaa ni kama kuhisi maumivu au kuhisi kichomi wakati wa kukojoa,kuongezeka kutokwa kwa majimaji ukeni,majimaji hayo ambayo ni ya njano au yaliyochanganyika n damu.



DK.Karen Jones kutoka hospital ya St.Jones alikaririwa katika mtandao wa health science akisema kuwa antbiotics ni miongoni mwa dawa nzuri zilizothibitika katika kutibu baadhi ya magonjwa ya zinaa kama kisonono na pangusa,ambazo hutoa majibu mazuri ikiwa zitatumiwa bila kukatishwa kwa dozi.
Mbali na magonjwa hayo pia kuna magonjwa kama kaswende,trichomoniasis,genitalwarts,ambayo yote huweza kutibiwa na antbiotics kwa usahihi.


Pia DK.Karen alishauri kuwa watu wenye  wapenzi  zaidi  ya mmoja wawe na tabia ya kwenda kupima magonjwa ya zinaa mara kwa mara ili kujua hli za afya zao.
Pia alishauri ikiwezekana waachene na vitendo vya kuwa na wapenzi zaidi ya mmoja au watumie Kondom ili kupunguza hatari ya maambukizi ya magonjwa ya zinaa.
Ifahamike kuwa magonjwa ya zinaa yakikaa mwilini kwa muda mrefu bila kutibiwa husababisha athari mbaya nyingi ikiwa ni pamoja na ugumba.  
  
                                
JIUNGE NASI , BONYEZA HAPA http://www.wabunifumedia.blogspot.com ku-install App ya wabunifumedia,  bila ya kuingia websiteTweet@wabunifumediaonline, youtube@wabunifumediaonline TV, Fb@wabunifumediaonline, insta@wabunifumediaonline                                                                                                                        

                                                                                                                                                            

Post a Comment

Theme images by Maliketh. Powered by Blogger.