Halloween party ideas 2015
Image

 Na Mwandishi wetu, Dar es salaam
TANZANIA ni nchi inayo ongozwa kwa misingi ya demokrasia na katiba, nchi yoyote ili iweze kusimama lazima iwe na katiba yake na wanachi pamoja na viongozi waitambue na kuilinda



                 Katiba ya Jamhuri ya Muungano  wa  Tanzania
                                    SEHEMU  YA  PILI
         MALENGO  MUHIMU NA MISINGI  YA MWELEKEO WA SHUGHULI ZA  KISERIKALI

Ufafanuzi Sheria ya 1984 Na.15ibara.6
6.Katika Sehemu ya Sura Hii,isipokuwa kama maelezo yahitaji vinginevyo “Serikai”
 Maana yake  ni pamoja na serikali ya Jamhuri ya Muuungano,Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar ,
 Serikali za mitaa na pia mtu anayetekeleza madaraka au mamlaka yoyote kwa niaba ya Serikali yoyote.
 Matumizi ya masharti ya sehemu ya pili.Sheria ya 1984           Na.15 ibara6
7-(1) Bila ya kujali masharti ya ibara ndogo ya
     (2),Serikali,Vyombo vyake na watu wote au mamlaka yoyote yenye kutekeleza madaraka ya utoaji
       Haki,watakuwa na majukumu na wajibu wa kuzingatia,kutia maanani na kutekeleza  masharti yote
       Ya sehemu hii ya surah ii.
     (2) Masharti ya sehemu hii ya surah ii hayataingiliwa nguvu ya kisheria na mahakama yoyote .kuamua
       Juu ya suala kama utendaji au kukosa kutenda sheria,au hukumu yoyote,inaambatana na masharti
        ya sehemu hii ya surah ii.
                    Serikali na watu ,sheria ya ujenzi na ujamaa na kujitegemea sharia ya 1984.na15.ibara.6 sheria 
                     na.4 ya 1992 ibara .6
 8-(1 )Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  ni nchi inayofuata misinginya demokrasia nah ski ya kijamii, na           
          Kwa hiyo-
      (a)wananchi ndio msingi wa mamlaka yote,na Serikali itapatikana madaraka na mamlaka yake yote,
           Na serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kwa mujibu wa katiba hii:
       (b)Lengo kuu la Serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi:
       (c)Serikali itawajibika kwa wananchi:
       (d)Wananchi watashirikiki katika shughuli  za serikali yao kwa mujibu wa masharti ya katiba hii
   (2) Muundo wa serikali ya jamhuri ya muungano  na serikali ya mapinduzi ya Zanzibar, au  wa cheo
         Chochote kati ya vyombo vyake na uendeshaji wa shughuli zakeutatelekezwa kwa kuzingatia umoja

      Wa jamhuri ya Muungano na haja ya kukuza umoja wa kitaifa na kudumisha heshima ya Taifa.


9.Lengo la katiba hii ni kuwezesha ujenzi wa Jamhuri ya Muungano na serikali ya mapinduzi Zanzibar au wa chochote kati ya vyombo vyake na ndugu na amani kutokana na kufuata siasa ya Ujamaaa na kujitegemea,ambayo inasisitiza utekelezaji wa misingi ya ujamaa kwa kuzingatia mazingira yaliyomo katika jamhuriya muungano.Kwa hiyo,Mamlaka ya Nnchi na vyombo vyake vyote vinawajibika kueleza sera na shughuli zake katika lengola kuhakikisha-
   (a);Kwamba utu na haki nyinginezo zote za binadamu zinaheshimiwa
    (b)Kwamba sheria za nchi zinalindwa na kutelekezwa;  
    (c)Kwamba shughuli za serikali zitatekelezwa kwa njia ambazo zitahakikisha kwamba utajili wa taifa
        Unaendelezwa ,unahifadhiwa na unatumiwa kwa manufaa ya wananchi wote kwa ujumla na pia
         Kuzuia   mtu kumnyonya mtu mwingine;
     (d)Kwamba maendeleo ya uchumi wa Taifa yanakuzwa na kupangwa kwa uangalifu na kwa pamoja;
      (e)  Kwamba  kila mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi anafanya kazi, na kazi maana yake ni shughuli
           Yoyote ya halali inayompatia mtu riziki yake;    
      (f)Kwamba heshima ya binadamu inahifadhiwa na kufuata Kanuni za Tangazo la Dunia Husika kuhusu
        Haki za binadamu;
     (g)Kwamba serikali na vyombo vyake vyote vya umma vinatoa nafasi zilizo  sawa kwa raia wote,wake   
        kwa waume ,bila ya kujali rangi,kabila,dini au hali ya mtu;
     (h)Kwamba aina zote za dhuluma,vitisho,ubaguzi,rushwa,uonevu na upendeleo zinaondolewa nchini;
      (i)Kwamba matumizi ya utajiri wa Taifa yanatilia mkazo  maendeleo ya wananchi na hasa zaidi
           Yanaelekezwa kwenye jitihada ya kuondosha umasikini,ujinga na maradhi;
     (j)Kwamba shughuli za uchumi haziendeshwi kwa njiazinazoweza kusababisha ulimbikizaji wa mali
         au njia kuu za chumi katika mamlaka ya watu wachache binafsi;
     (k)Kwamba nchi inatawaliwa kwa kufuata misingi ya kidemokrasia au ujamaa;
                                Nafasi na mamlaka ya chama sharia ya 1984.Na.15.ibara6
10.[ibara ya 10 ya katiba imefutwa na sharia na.4 ya 19920)
Itaendelea..


JIUNGE NASI , BONYEZA HAPA http://www.wabunifumedia.blogspot.com ku-install App ya wabunifumedia,  bila ya kuingia websiteTweet@wabunifumediaonline, youtube@wabunifumediaonline TV, Fb@wabunifumediaonline, insta@wabunifumediaonline

Post a Comment

Theme images by Maliketh. Powered by Blogger.