Halloween party ideas 2015
Image

MMILIKI WA TP MAZEMBE AHUKUMIWA KWENDA JELA.

Na Yusuph Mwamba

MMILIKI wa klabu ya Soka ya  TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Moise
Katumbi,amehukumiwa kwenda jela miaka mitatu.
Moise Katumbi

Kufuwatia kuhukumiwa kwa Katumbi mika mitatu, kuna kwenda  sambamba na kutozwa faini ya dola milioni 6 kwa kosa la kujimilikisha eneo.

Rais huyo wa TP Mazembe, pia alikuwa na dhamira ya  kugombea nafasi ya Urais wa Kongo katika uchaguzi unaotarajia kufanyika mwisho wa mwaka 2016 kupita  chama cha upinzani kushindana na Rais anayekaribia kumaliza muda wake kwa awamu  ya sasa   Rais Joseph Kabila.

Hata hivyo, wakati hukumu hiyo ikitolewa,Moise  Katumbi, alikuwa hayupo Nchini Congo, alikuwa akasafiri kuelekea  Afrika Kusini kupata matibabu.

Baadhi ya makosa mengine yaliyompelekea Katumbi kuhukumiwa jela ,  ni pamoja na swala la kuajiri  wa geni kutoka nje ya Kongo kwa ajili ya kuandaa njama za kumuondoa
Rais Kabila katika kinyang`anyiro cha kugombea Urais wa Nchi hiyo..
Moise Katumbi akisalimiana na wachezaji wake

Miongoni mwa mafaniko aliyoyapata Moise Katumbi ni pamoja na kuwa Rais wa kwanza wa klabu ya TP Mazembe aliyeiongoza klabu hiyo kucheza hatua ya fainali ya klabu bingwa ya Dunia dhidi ya klabu ya Inter Milan desemba 18, 2010 ,ikiwa chini ya Jose Morinho, rekodi ambayo imeifanya TP Mazemba kuwa klabu pekee Barani Afrika kufikia hatua hiyo, na sasa Mazembe wanakuja Tanzania kucheza mchezo wao wa pili wa nane bora dhidi ya Yanga, mchezo utakao pigwa juni 29, 2016 kwenye Uwanja wa Taifa Dar Es saalam majira ya saa moja usiku.  
Wachezaji wa TP Mazembe wakishangilia goli katika moja ya mchezo wao

Katumbi akiwa kwenye mahojiano maalumu na waandishi wa habari




Post a Comment

Theme images by Maliketh. Powered by Blogger.