Na Mwanaid Mziray (Tsj) Dar es salaam
AFISA
Kitengo cha Chakula ,maji salama na mazingira kutoka Wizara ya afya, jamii,
wazee, jinsia na watoto,Stephen Kiberiti, ameishauri jamii kuwa makini juu ya
uhifadhi wa vyakula na kuepuka kutumia
mifuko ya plastiki kuhifadhi chakula.
Akizungumza
nagazeti hili ofisini kwake,Kiberiti alisema anaishauri jamii kuhakikisha
maeneo ambayo yanauzwa chakula ni safi na salama kwa afya, ikiwa ni pamoja na
kuhifadhi chakula katika mazingira yanayo hitajika.
“Nawashauri wanajamii
wawe makini juu ya kuhifadhi vyakula na mazingira katika hali ya usafi na usalama
kwa matumizi na afya kwa ujumla,”alisema Kiberiti
Aidha
aliongeza kusema kwa kuitaka jamii kuhifadhi
vyakula katika mazingira yanayohitajika ili kuepukana na magonjwa
hatarishi yenye kuambukiza kama vile homa za matumbo,kipindupindu na kuharisha.
Licha ya
hivyo aliwaomba viongozi wa halmashari kuendelea kutumia sheria ndogo ndogo ili
kudhibiti uchafuzi wa mazingira na kutoa elimu kwa jamii juu ya athari
zitokanazo na mazingira kuwa machafu na namna ya kuepukana nayo kwa usalama wa
afya zao.
“Hii sio
kwamba tunawakatili wananchi ni kwajili ya kuweza kuona namna ya kuondokana na
magonjwa hatarishi yasiyo ya lazima yanayoweza kuepukika,” alisema Kiberiti.
IUNGE NASI , BONYEZA
HAPA http://www.wabunifumedia.blogspot.com ku-install App ya wabunifumedia, bila ya kuingia website
Tweet@wabunifumediaonline, youtube@wabunifumediaonline TV, Fb@wabunifumediaonline, insta@wabunifumediaonline .
Tweet@wabunifumediaonline, youtube@wabunifumediaonline TV, Fb@wabunifumediaonline, insta@wabunifumediaonline .
Post a Comment