WAKATI tetesi na harakati za usajili zikiwa zinaendelea kushika kasi Bara Ulaya na kila pembe ya Dunia ,ikiwa ni kuzifanya klabu kuimarisha vikosi vyao kabla ya kuelekea kuanza kwa misimu , uwezo na ushirikiano aliouonesha nyota mpya wa Chelsea N'Golo Kante , pengine umeufanya klabu hiyo kujiweka kifua mbele na kuwa usajili wenye tija kunako klabu hiyo yenye makazi yake Stamford Bridge.



Kante , alifanikiwa kuingoza klabua ya soka ya Leicester City na kuchukua ubingwa wa ligi kuu ya Uingereza msimu wa 2015/16, huku akiwa ametengeneza ngome ngumu katika safu ya ulinzi na kuifanya klabu hiyo kuwa bora kutokana na kujiamni
(confidense) kwake na kuongeza mafanikio ya klabu hiyo kabla ya kuanza kwa msimu.
Kwa maana hiyo, kuja kwa Kante, kutaifanya klabu hiyo kubadili mfumo (formation) wa uchezaji waliokuwa wakicheza msimu uliopita na kuifanya klabu hiyo iwe na ulinzi zaidi kwa kutumia mfumo wa 4-1-4-1 kutoka 4-4-2 waliokuwa wakiutumia mwanzo.
JIUNGE NASI , BONYEZA HAPA http://www.wabunifumedia.blogspot.com ku-install App ya wabunifumedia, bila ya kuingia websiteTweet@wabunifumediaonline, youtube@wabunifumediaonline TV, Fb@wabunifumediaonline, insta@wabunifumediaonline
Post a Comment