Na Yusuph Mwamba
“Michango ya wabunge wa upinzani ina umuhimu mkubwa hasa katika mijadala ya kupitisha bajeti ya Nchi, ambayo pia inagusa katika majimbo yao, sasa basi kutoka nje ya Bunge si njia pekee ya kutatua matatizo kwa kuwa ndani ya vikao hivyo ndipo zinapojadiliwa changamoto mbalimbali za majimbo yao ambayo yote yanategemea Bajeti kuu, ni vema warudi hatua stahiki zitachukuliwa kufanya hivyo wanawanyima haki waliowachagua".Alisema Mangula
Aidha, alisisitizia suala la kususia vikao na kwenda kuijadili bajeti nje ya Bunge hakutaweza kuleta manufaa kwa Taifa na hata kwenye majimbo yao na baadala yake warudi Bungeni kuendelea na masuala ya kitaifa yanayoendelea hivi sasa.
Akizungumzia suala la adhabu walizopewa wabunge saba wa upinzani, Mangula alisema kila jambo lina utaratibu na kanuni zake za kufuata kwahiyo kwa Mbunge yeyote atakaye kwenda kinyume na maadili ya Bunge na kutofuata kanuni na sheria adhabu lazima imwangukie haijalishi Upinzani wala chama tawala kincoangaliwa ni haki kwa wa Wabunge wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
![]() |
Makamu mwenyekiti CCM Taifa Phillip Mangula akifafanua jambo juu ya Wapinzani kugomea Bajeti |
Post a Comment