Halloween party ideas 2015
Image

Na Mwandishi wetu
Chabanga Hassan Dyamwale amefariki dunia asubuhi ya leo katika hospitali ya Muhimbili, Dar es Salaam alipokuwa amelazwa kwa matibabu


Na Ngade amesema kwamba mazishi yanaweza kuchelewa hadi mtoto mwingine wa marehemu, Mamdoe anayeishi Marekani awasili Jumanne. “Kuna uwezekano mkubwa marehemu akasafirishwa Jumatano mapema kwa mazishi yatakayofanyika Handeni,”amesema.  

Ngade amesema baba yao ameacha wake wawili, Asha na Mboni na watoto tisa, ambao pamoja na yeye mwenyewe na Mamdoe, wengine ni Ibrahim, Mwanahija, Yahya, Mkufu, Makileo, Mkebene na Juma. 

Umaarufu wa marehemu ulianzia kwenye mchezo wa Riadha na aliwahi kuiwakilisha Tanzania kwenye Michezo ya Olimpiki mwaka 1964 nchini Japan wakati huo akiwa na umri wa miaka 23 akiwa na akina Psacal Mfyomi, Daniel Thomas na Omar Abdallah.

Ndiye aliyefanikisha mfumo wa ufutaji madeni ya FAT aliouita OFUMA na akaanzisha Ligi ya timu sita zikiwemo Yanga, Simba, Coastal Union, African Sports, Pamba zilizocheza ligi hiyo Uwanja wa Taifa (sasa Uhuru) na kufanikiwa kulipa madeni. 

Awali kabla ya kuanzisha ligi hiyo, aliulizwa na baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (sasa marehemu) ataondoaje madeni ya FAT akamweleza mipangilio yake na kupewa Kombe la ushindani na Mwalimu Nyerere ambalo lilibebwa na Coastal Union, kipindi hicho Waziri wa Michezo alikuwa Jenerali Mirisho Sarakikya.
Ni Sarakikya aliyempeleka Dyamwale kuwa Katibu wa Chama cha Soka Tanzania (FAT), chini ya Mwenyekiti Alhaj Said El Maamry kuanzia miaka ya 1970. Aliondoka FAT mwaka 1978 na akaenda kuwa Mkurugenzi wa Michezo nchini mwanzoni mwa miaka ya 1980.
Mzee Dyamwale ambaye aliwahi pia kuwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii alikuwa mpenzi na mwanachama wa klabu ya Yanga. Mungu ampumzishe kwa amani marehemu Hassan Chabanga Dyamwale. Amin.

Post a Comment

Theme images by Maliketh. Powered by Blogger.