Halloween party ideas 2015
Image

Na Tatu Muhamed
 
KATIBU Mkuu  wa Wizara ya Maji Prof. Kitila Mkumbo amesema kuwa hakuna sababu ya  taasisi za Serikali kushindwa kulipa bili ya maji wakati taasisi hizo zinapewa fedha kutokana serikalini ikiwa watu wenye hali ya chini wanalipa.
Aidha Prof. Kitila, amesema kazi kubwa inayotakiwa kufanyika kwasasa ni kuhakikisha miradi yote inamalizika kwa haraka ili wahitaji wa maji waweze kuhudumiwa bila matatizo yoyote.
 
Profesa Mkumbo, ameyasema hayo jana katika ziara yake ya kwanza tangu alipoteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa wizara ya maji, ambapo pamoja na mambo mengine aliipongeza Dawasco kwa kazi kubwa wanayoifanya  kwani ukilinganisha na huko nyuma ambapo malalamiko ya maji  yamepungaua kwa kiasi kikubwa.
 
 
Prof. Mkumbo amesema haiwezikani  mwananchi wa kawaida  anamudu kulipa  bili ya maji halafu taasisi za serikali ambazo zinapewa fedha zinashindwa kulipa hivyo lazima wahakikishe wanalipa na Dawasco wanatakiwa wafanye kazi hiyo ya kukusanya bili hizo za maji.
 
’Nawapongeza  Dawasco  kwani mnafanya kazi kubwa  binafsi nimekuwa nikiwafuatilia hata kabla sijaingia wizarani kwakweli mnafanya kazi kubwa na mnastahli kupongezwa  lakini muendelee hivyo na kwakweli wananchi wanataka maji si vinginevyo, " amesema Mkumbo na kuongeza kuwa: 
 
"Wananchi wa kawaida wenye kipato cha chini wanalipa iweje kuwe na Taasisi ambazo hazilipi?. Ni lazima walipe, Rais aliposema Taasisi zisizolipa umeme zikatiwe, hakumaanisha umeme pekee.... Tunahitaji pesa kuwekeza kwenye miundombinu na Taasisi zote zinabajeti za kulipa bili, kwahiyo zilipe, " amesema Prof Mkumbo.
 
Aidha Prof. Mkumbo, amesema pamoja na kazi kubwa katika kufanikisha swala la maji linakuwa historia, amesema  kuwa watoke kwenye lengo  badala yake  wahakikishe tatizo la maji linakwisha kabla ya kufika 2020  kwani kuna miradi mikubwa mno ya maji ambayo inatekelezwa na kama ikikamilika basi shida ya maji itakuwa imepata suluhisho.
 
Mkumbo aliongeza kuwa lazima shirika litoke kwenye mtazamo na kuingia kwenye uhalisia  na hiyo ndiyo kazi kubwa  iliyopo  na hapo nikuona watu wanapata maji  huku kibainisha maeneo kama Bonyokwa,Pugu,Chanyanyikeni Kinyerezi, maeneo hayo kwa kiasi kikubwa yanakabiliwa na Changamoto kubwa ya maji na yeye kama Katibu amepongeza Dawasco kwa kuliona hilo.
 
Pro. Mkumbo, amesema ni aibu kuona katika kipindi cha miaka 50 bado kuna tatizo la maji  hivyo  lazima wakimbie mbio  na huo ndio utakuwa ugomvi wake mkubwa kwa watendaji na atahakikisha anawasumbua mno lakini lengo kuona wananchi wanapata maji.
 
Awali akitoa uwasilishaji wake  kwa katibu huyo Ofisa Mtendaji mkuu wa Dawasco  Sypriani Luhemeja, Prof. Mkumbo, amesema kuwa shirika hilo limepiga hatua kubwa ukilinganishana na huko nyuma ambapo uzalishaji ulikuwa chini.
 
Alisema hivi sasa Dawasco wanazalisha lita milioni 480 kwa siku na hitaji ni milioni 512  nakudai kuwa kiwango hicho ni kikubwa ukilinganisha na huko nyuma na kwamba bado wamejipanga kikamilifu kuhakikisha kwamba wanamaliza tatizo la maji katika mkoa wa Dar es Salaama na Pwani.
 
Aidha amefafanua kuwa uzalishaji wa maji  katika ruvu chini ni lita milioni 217 ,ruvu juu lita mil, 196  na kutoka mtoni lita 9000 na vyazo vinginevyo vinachangia kwa asilimi ndogo  huku akibainisha kuwa jumla ya wateja  187,087  wamehudumiwa   na lengo nikuwafikia wateja 400000, ifikapo mwezi  juni 2017.
 
Akizungumzia Changamoto za shirika hilo, Luhemeja amesema ni usambazaji wa maji pamoja na upotevu wa maji  ambapo katika kipindi cha mwaka 2015 maji yalipotea kwa asilimia 57 na kufikia mwezi machi mwaka huu maji yamepotea kwa asilimia 37.8.
 
JIUNGE NASI , BONYEZA HAPA http://www.wabunifumedia.blogspot.com ku-install App ya wabunifumedia,  bila ya kuingia website
Tweet@wabunifumediaonline, youtube@wabunifumediaonline TV, Fb@wabunifumediaonline, insta@wabunifumediaonline
 
 

Post a Comment

Theme images by Maliketh. Powered by Blogger.