Halloween party ideas 2015
Image

Na. Zephania. j kapaya

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) inasema ina mpango wa kuwaongezea wazee waliofikia umri wa miaka 70 fedha za pensheni jamii zinazotolewa kila mwezi, endapo vyanzo vyake vya kukusanyia mapato vitaimarika au hali itakapo ruhusu.
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Wazee,Ustawi wa Jamii Zanzibar, Mhaza Harib Juma, amesema kufuatia malalamiko ya wazee kuwa pesa wanayopewa na serikali kila mwezi haikidhi mahitaji yao, amewataka wafanyabiashara kulipa kodi kwa wakati na wananchi kudai risiti wanaponunua bidhaa ili mapato yaweze kuongezeka na kuiwezesha serikali kufanikisha suala hilo la kuongeza pensheni jamii.
Amesema endapo serikali itakusanya kodi vizuri kupitia vyanzo vyake vya mapato, pensheni hiyo itaweza kuongezwa nakuwataka wazee kuwa wastahamilivu na waridhie na pesa wanazopokea kila mwezi hivi sasa.
Aidha Mhaza ametoa ushauri kwa watoto wa wazee wanaopokea pensheni jamii kuzifanyia biashara fedha hizo ili ziweze kujizalisha na kuweza kukidhi mahitaji ya wazee wao na kuwacha tabia ya kuzitumia fedha hizo kwa mahitaji yao binafsi.
Hata hivyo amesema serikali inalengo zuri la kuwasaidia wazee waliofikia miaka 70 kutokana na kuthamini juhudi na michango yao kwa taifa.
Zaidi ya wazee 27,000 waliofika umri wa miaka 70 wanafaidika na pensheni jamiii, ambayo ni shilingi 20,000 kwa mwezi inayotolewa na serikali tokea April 2016 mwaka jana.

Post a Comment

Theme images by Maliketh. Powered by Blogger.