Halloween party ideas 2015
Image


Na Shayda kadiri 
BINADAMU kwa kawaida miili yetu imeumbwa ikiwa na vimeng’enya ambavyo husaidia kuvunja vunja chakula ili kiweze kusagwa, vimeng’enyaji hivi vipo kuanzia mdomoni na njia yote ambapo chakula kinapita hadi kwenye utumbo mdogo ambapo ufyonzaji wa viini lishe hufanyika. Moja ya kimeng’enyaji  kinachopatikana tumboni ni asidi ama tindikali  inayoitwa hydrochloric acid ( HCL) .Asidi hii humwagwa juu ya chakula ili kurahisisha usagaji wa chakula tumboni. Kupanda kwa tindikali ni tatizo kubwa kiafya, ambalo linathiri watu wengi sana.
 Kuna wakati umewahi kupatwa na hii hali kwamba unapocheua basi unaona kama kuna maji maji yenye uchachu yanapanda kutoka tumboni adi kwenye koromeo, kitendo hichi ndicho tunaita KIUNGULIA. Hapo zamani  ilifahamika kwamba tatzo hili hutokana na wingi wa tindikali tumboni ndio maana wagonjwa hupewa dawa zinazohuisha asidi hiyo.



NINI KINACHOSABABISHA KIUNGULIA?

Chakula kinapopita kutoka kwenye tumbo dogo (esophagus) na kuingia kwenye mfuko mkubwa wa tumbo basi valve za chini hufunga ili kuzuia chakula na tindikali  visirudi tena, na ndio maana hata mtu akila mda huo huo ukamuweka miguu juu mikono chini chakula hakitoki. Kiungulia hutokea pale misuli midigo au valve zinaposinyaa na kuruusu aside iliyopo tumboni  kurudi mpaka kwenye tumbo dogo (esophagus) .

Lakini ni muhimu sana kufahamu  kwamba tatizo la kurudi  kwa tindikali halisababishwi na wingi wa tindikali kwenye tumbo ila ni dalili zinazoletekezwa na  Madhara ya bacteria waitwao Helicobacter pylori (H.pylori)  inakadiriwa kuwa zaidi ya nusu ya watu duniani wameathiriwa na H.pylori
 

JE UNAPATA MADHARA KUTOKANA NA MATUMIZI VIDONGE???
kama kiungulia chako kinasababishwa na dawa unazomeza  basi  jibu ni kwamba namna ya kujikinga kiungulia ni kuwa makini jinsi unavotumia vidonge, lini unatumia na pia unatumiaje vidonge au dawa hizo. Hakikisha usiongeze tena vidonge vingine kwa ajili ya kuhuisha hali hiyo pale inaposababishwa na matumizi ya dawa. Hizi ni baadhi ya njia ambazo zitaweza kukusaidia kupunguza makali ya kiungulia
       Epuka kutumia dozi zaidi ya ile uliyoshauriwa na dactari
       Baadhi ya dawa ni vizuri zikamezwa tumbo likiwa tupu halina chakula na zingine humezwa hata tumbo likiwa na chakula, hivyo hakikisha unasoma kwanza maelezo kwenye kipeperushu ndani ya dawa au muulize dactari au muhudumu akupe ushauri jinsi na lini kuweza kutumia dawa
       Muulize dactari au muhudumu kupiia dawa na virutubisho vyote unavyotumia kama vinasababisha kiungulia
       Tumia chai ya Tangawizi.
TIBA YAKO YA KWANZA NI VYAKULA VYA ASILI AMBAVYO HAVIJASINDIKWA
Siri kubwa ambayo itakusaidia kutatua tatizo la kiungulia na asidi ni kurudisha matumizi ya vyakula vya asili ili kufanya tumbo liweze kufanya kazi katika hali yake ya kawaida. Ukweli ni kwamba matumizi makubwa ya vyakula vilivyosindikwa  na sukari ni njia isiyopingika kabisa iko wazi kwamba inasababisha kiungulia na tindikali kuwa nyingi kutokana na kitendo hicho kuvuruga mpangilio wa bacteria wazuri waliopo tumboni na kwenye utumbo.
Badala yake hakikisha unatumia zaidi mbogamboga na vyakula vingine visivyosindikwa vilivyo na ubora, Epuka vyakula  na vinywaji vyenye Caffeine,pombe, na nicotine. 
Kitu kingine cha muhimu hakikisha unatengeneza bacteria wengi wazuri kutoka kwenye mlo wako. , Hii itasaidia kutengeneza mazingira ya asili kwa ajili ya umeng’enyaji wa chakula na pia kusaidia kuondoa bacteria wabaya wanaosababisha vidonda vya tumbo ambao huitwa H.pylori bila hata kutumia dawa.Pia ulaji wa vyakula vya asili unasaidia kurahisisha usagaji wa chakula na ufyonzaji wa viini lishe katika damu.

NJIA ZINGINE AMBAZO NI SALAMA NA ZA UHAKIKA KATIKA KUTIBU TATIZO LA KIUNGULIA  NA KUPANDA KWA TINDIKALI YA TUMBONI.

       CHAI YA TANGAWIZI, tangawizi inajulikana kutokana na uwezo wake mkubwa wa kuua bacteria na kutatua tatizo la asidi kujaa tumboni. Changanya vipande viwili au vitatu vya tangawizi vilivyopongwa ndani ya vikombe  viwili vya maji ya moto kasha acha kwa nusu saa kasha kunywa dakika 20 au 30 kabla ya mlo wako. 
       VITAMINI D, vitamin D ni muhimu katika kutatua athari zozote zile ndani ya mwili, unaweza kupata vitamin D kwa kupata mwanga wa jua la asubuhi au la jioni, kwa kupata usingizi mzuri. Lakini kutokana na kuwa unaweza kuwa bize na kazi zako basi tutakupatia kirutubisho cha asili kabisa, 
       GLUTAMINE, tafiti zilizofanyika mwaka 2009 zinaonyesha kwamba matatizo mengi ya tumbo yanayosababishwa na bacteria wa H.pylori yanahusishwa na upungufu  amino aside inayoitwa Glutamine ambayo hupatikana kwenye vyakula vingi kama nyama, kuku, samaki, mayai, na baadhi ya matunda na mbogamboga.
      VITAMINI B9 (FOLIC ACID) NA VITAMINI B ZINGINE, Tafiti zinasema vitamin B zinapunguza uwezekano wa kupanda kwa tindikali. Matumizi mazuri ya Folic acid basi yanweza kupinguza hali ya kiungulia kwa karibu 40%
       JUISI YA ALOE VERA,  mmea wa aloe unafahamika kwa uwezo wake mkubwa wa kuponya vidonda vya tumbo na kuondoa tatizo la mrundikano wa tindikali na gesi tumboni. Kunywa vikombe viwili vya juisi ya aloce vera kabla ya kula chakula. ANGALIZO cyo kila mmea wa Aloe vera una dawa inayotakiwa ndani yake kuna aina baadhi ya mimea ya dawa. Kama huwezi kupata mmea huo basi  tutakupatia kirutumbisho  kilichopo katika mfumo wa vidonge. Usitumie dawa zenye sumu


J   JIUNGE NASI , BONYEZA HAPA http://www.wabunifumedia.blogspot.com ku-install App ya wabunifumedia,  bila ya kuingia websiteTweet@wabunifumediaonline, youtube@wabunifumediaonline TV, Fb@wabunifumediaonline, insta@wabunifumediaonline




.



Post a Comment

Theme images by Maliketh. Powered by Blogger.