Halloween party ideas 2015
Image

Na Yusuph Mwamba

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema kwamba Mkutano Mkuu Maalumu wa chama hicho, utakaofanyika mwishoni mwa wiki hii si wa kupokezana vijiti, kwa sababu nafasi za Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti unapofika wakati wa uchaguzi haziombwi, bali yanapendekezwa majina ya watu wanaofaa kushika nyadhifa huo.





Hata hivyo, chama hicho kimesema kuwa, maandalizi ya mkutano huo utakaofanyika Jumamosi wiki hii, yamekamilika na unatarajiwa kushirikisha wajumbe wapatao 2,456 na mpaka sasa wamekodi jumla ya  hoteli 306 ambazo zitawalaza zaidi ya watu 3,331 mjini Dodoma.





Akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wake jana,Mkuu w kitengo cha habari wa CCM, Christopher ole Sendeka alisema kuwa ,Mkutano Mkuu Maalumu wa Taifa utamchagua Mwenyekiti wa CCM Taifa baada ya Mwenyekiti wa sasa anayetarajia kumaliza muda wake na Rais mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa awamu ya nne,Dr Jakaya Kikwete kung’atuka na kutoa nafasi hiyo kwa Rais wa awamu ya tano, Dr John Magufuli kugombea nafasi hiyo baada ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Kikwete.




Aidha, amesema kuwa , Rais Magufuli atakuwa Mwenyekiti wa CCM wa tano wa mujibu wa Katiba ya CCM, nafasi ya Mwenyekiti wa CCM na Makamu Mwenyekiti wawili unapofikia wakati wa uchaguzi nafasi hizi haziombwi isipokuwa Kamati Kuu ya Taifa ya CCM inafikiria na kupendekeza majina na kuyawasilisha kwa Halmashauri Kuu ya Taifa ambayo humteua,” alisema Sendeka.

Alisema kisha Mkutano Mkuu wa Taifa unamchagua kwa kumpigia kura. 

Alisema wanaopendekezwa hawajazi fomu za kugombea nafasi hizo na katika mchakato huo kinachofanyika si kupokezana kijiti, kama wengi wanavyopenda kuita, bali ni uchaguzi wa kumpata mwenyekiti wa CCM.

Aliongeza kuwa, katika uchaguzi huo itapigwa kura ya ‘ndio’ au ‘hapana’ ili kupata mwenyekiti na lazima apate nusu ya kura na akipata chini ya nusu mapendekezo yataanza upya.

“Tuna imani wajumbe wote watampa mwenyekiti mpya kura zote za ‘ndio’ ili achukue nafasi ya kuongoza kitaifa,” alisema na kuongeza kuwa akipatikana mwenyekiti ataunda ‘jeshi’ lake, kwani hiyo ni desturi ya chama na walio katika Sektetarieti, watapisha ili mwenyekiti mpya aunde jeshi lake.



Rais Magufuli, anatarajiwa kufanya mabadiliko makubwa ya uongozi ndani ya CCM baada ya kukabidhiwa uenyekiti wa Taifa, kwa kupanga upya safu yake ya viongozi, ambao anaamini anaweza kufanya kazi nao kwa ajili ya kuleta mabadiliko ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM)


 JIUNGE NASI , BONYEZA HAPA http://www.wabunifumedia.blogspot.com ku-install App ya wabunifumedia,  bila ya kuingia website

Tweet@wabunifumediaonline, youtube@wabunifumediaonline TV, Fb@wabunifumediaonline, insta@wabunifumediaonline



Post a Comment

Theme images by Maliketh. Powered by Blogger.