Halloween party ideas 2015
Image




Na Zephania Kapaya

Watanzania wametakiwa kuhudhuria semina ya ufunguzi wa onesho la chimbuko la Binadamu wa Afrika  ikiwa ni onesho na matokeo ya tafiti mbalimbali zilizofanyika bonde la Olduvai na Laetoti hifadhi ya mamlaka ya Ngorongoro.

Hayo yamesemwa na Prof.Audax Mabula ambaye ni mkurugenzi wa Makumbusho Taifa ambapo ameekeza kuwa  Makumbusho ya ya Taifa ikishirikiana na ubalozi wa Spain Tanzania,Makumbusho ya Aikolojia ya Madrid,Taasisi ya chimbuko la Binadamu(IDEA) Madrid,Chuo kikuu cha Acla Madrid na Makumbusho ya Cosmocaixa Barcelona- Spain na kampuni ya siment ndio waliondaa onesho hilo wakiwa na lengo la kuwaonesha na kuwafunza watu mbalimbali kuhusiana na chimbuko la Binadamu Afrika.

Aidha Prof.Mabula amesema mgeni rasmi katika onesho hilo ni Waziri wa Maliasili na Utalii Dr Hamis Kigwangwalla na litazinduliwa saa 11:00 jioni Makumbusho ya Taifa jijini dar es salaam na wageni mbalimbali wanatariwa kuwepo wakiwamo Mabalozi,wananchi,na viongozi mbakimbali.

Prof.Mabula ameendelea kwa kusema kuwa vionyeshwa vyote katika onesho hilo vimepatikana hapa Tanzania kutokana na tafiti za kisayansi na vimehifadhiwa Makumbusho ya Taifa vioneshwa hivo ni pamoja na Masalia ya Zamadamu,Zana za Mawe na Masalia ya Wanyama walioishi takribani tangu milioni 4 iliyopita.

Prof Mabula amemaliza kwa kuwataka wananchi wote kuhudhuria kwa wingi  katika onesho hilo pamoja na semina kwani hakuna kiingilio na kwa siku ya pili kiingilio kwa MTU mzma ni shilingi 1500,mtoto ni shilingi500.
Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Post a Comment

Theme images by Maliketh. Powered by Blogger.